Selamawit ana umri wa miaka 29. Alimzaa mwanae wa kwanza nchini Eritrea. Yeye na familia yake walikuwa na maisha magumu huko, kwa hiyo wakaamua kwenda Italia.
Selamawit is 29 years old. She gave birth to her first child in Eritrea. She and her family had a hard time there, so they decided to go to Italy.
Inga aliondoka nyumbani kabla hajafikisha miaka 19. Alienda Norwei na akapata mwanae wa kwanza huko.
Inga left home just before she turned 19. She moved to Norway and had her first child there.
Wakati Selamawit alipopata ujauzito wa mtoto wake wa pili, alistaajabu jinsi itakavyokuwa kujifungua mtoto katika nchi tofauti.
When Selamawit became pregnant with her second child, she wondered what it would be like to have a child in a different country.
Selamawit na Inga wana tajiriba tofauti. Selamawit alihisi yuko salama kwa sababu ana uzoefu wa kujifungua. Inga alizungumza na mama yake kuhusu kujifungua.
Selamawit and Inga come from different backgrounds. Selamawit felt safe because she had experience with giving birth. Inga talked to her mother about giving birth.
Wanawake wote wawili walifahamu kwamba katika mataifa mengi ya Ulaya, wanawake wajawazito wana haki ya kupata huduma za afya. Hii inamaanisha kwamba watapata msaada wakati wa ujauzito wao. Selamawit alipanga miadi na daktari wake mara tu baada ya kugundua kuwa ni mjamzito. Mume wa Selamawit alimpeleka kwa daktari.
Both women had heard that, in most European countries, pregnant women have the right to antenatal care. This means that they will get help during their pregnancies. Selamawit made an appointment with her doctor as soon as she realised she was pregnant. Selamawit’s husband drove her to the doctor.
Daktari alifanya baadhi ya vipimo na akagundua kuwa Selamawit ana aina fulani ya kisukari ambacho wanawake wengi wajawazito hupata. Alipaswa kula vyakula vyenye virutubisho na kufanya mazoezi. Selamawit alifurahi kwani alienda kwa daktari mapema kabla yeye na mtoto wake kuugua.
The doctor did some tests and found out that Selamawit had a kind of diabetes that some pregnant women get. She had to eat healthy food and exercise. Selamawit was glad she went to the doctor early, before she and her baby became ill.
Baada ya jirani wa Inga kusikia kwamba anajaribu kupata mtoto, akamshauri amuone daktari mara tu baada ya kugundua kuwa ni mjamzito. Kwa kufanya hivyo, angeweza kuwa na uhakika kwamba yeye na mtoto wake wangekuwa na afya njema. Daktari akamwambia anywe vidonge vya wajawazito vina vitamini muhimu kwa wanawake wajawazito.
When Inga’s neighbour heard that she was trying to have a baby, the neighbour told her to see a doctor as soon as she was pregnant. That way she could make sure that she and her baby were healthy. The doctor told her to take folic acid, a vitamin that is important for pregnant women.
Inga na daktari wake walikubaliana kwamba aonane na mkunga kwa ajili ya vipimo vya mara kwa mara wakati wote wa ujauzito. Mkunga alimpa ushauri kuhusu chakula, kupumzika, na taarifa za jinsi ya kujilinda vizuri yeye na mtoto wake.
Inga and her doctor agreed that she would meet a midwife for regular check-ups during her pregnancy. The midwife gave her advice on food and rest, and information on how to keep herself and her baby safe and well.
Wanawake wote wawili walijifungua watoto wenye afya bora. Selamawit alipata mtoto mwingine wa kiume wakati Inga alipata mtoto wa kike. Waume zao walihisi fahari na walimwambia kila mtu waliyemjua kuhusu wake zao imara na watoto wao wenye afya bora.
Both women gave birth to healthy babies. Selamawit had another son, while Inga had a daughter. Their husbands were very proud, and they told everyone they knew about their strong wives and healthy children.