Mimi na kaka zangu wawili tulikuja Norwei mwezi Disemba 2016. Tulivaa nguo za majira ya joto kwa sababu tulifikiri Norwei kutakuwa na joto kama Somalia. Hata hivyo, tulipofika uwanja wa ndege kulikuwa na theluji. Tulihisi baridi na hali ya hewa ilikuwa ya baridi sana. Ingawa tulibeba mabegi, yalikuwa na nguo za majira ya joto tu.
My two brothers and I came to Norway in December 2016. We wore summer clothes because we thought it would be as warm in Norway as it was in Somalia. However, when we arrived at the airport, it was snowing. We were cold and the weather was chilly. Although we had brought a few suitcases, they only had summer clothes in them.
Hata kama kulikuwa na baridi, nilifurahi sana tulipokuja Norwei. Hatimaye niliweza kufanikiwa kuonana tena na mama yangu ambaye sikumuona kwa miaka sita. Tulionana na mama pamoja na rafiki zake wawili. Tulipomuona tulilia kwa furaha. Tulienda kwenye mji mdogo ambapo mama anaishi.
Even though it was cold, I was very happy when we came to Norway. I would finally meet my mum again, whom I had not seen for six years. My mum and two of her friends met us. When we saw her, we wept with joy. We drove to the small town where Mum lives.
Siku za mwanzo tukiwa katika mji wa mama zilikuwa ni za kustaajabisha. Kulikuwa na baridi na theluji na hatukuweza kuona chochote. Mitaa ilikuwa tupu kabisa. Watu wachache niliokutana nao walionekana wakihisi baridi na hawakuwa sawa. Somalia kulikuwa na watu kila mahali, kwa hiyo kila kitu kilikuwa kigeni hapa. Mama yangu na rafiki zake walitupatia zawadi na kisha akatupeleka kununua nguo za majira ya baridi.
The first days in Mum’s town were very strange. It was cold and snowy and there was not much to see. The streets were completely empty. The few people I met seemed cold and unfriendly. In Somalia there were people everywhere, so everything felt unfamiliar here. My mum and her friends gave us some presents, and then she took us to buy winter clothes.
Baada ya mapumziko ya Krismasi, nilijiunga na kozi ya Kinorwei katika kituo cha elimu ya watu wazima. Nilisoma pale kwa muda wa miaka miwili kabla ya kuanza shule ya msingi. Sasa nipo mwaka wa mwisho na nimejitengenezea marafiki wengi. Ninapenda sana kuongea na watu na kufurahia kuonana na watu wapya.
After the Christmas holidays I joined a Norwegian course at the adult education centre. I studied there for two years before starting in an ordinary school. Now I am in my final year, and I have made many new friends. I am very sociable and enjoy meeting other people.
Baada ya masomo, huwa ninaenda kwenye kituo kinachoendeshwa na wajitoleaji ambapo huwa ninasaidiwa kufanya kazi ya nyumbani. Pia nimejiunga na kozi ya kushona katika kituo hiki.
After school I go to a centre run by volunteers where I get help with my homework. I have also joined a sewing course at the centre.
Nilipokuwa Somalia, sikuwahi kwenda shule au kujiunga na kozi yoyote isipokuwa shule ya Kuran. Sikujua kusoma wala kuandika. Sasa nimeshajifunza namna ya kuandika Kisomali na Kinorwei na masomo mengine mengi. Bila elimu, nilijihisi si kitu. Sasa ninajiona mwenye maarifa na furaha.
In Somalia I never went to school or did any courses except Quran school. I did not know how to read or write. Now I have learned how to write in both Somali and Norwegian, and many other subjects. Without education I felt I was nobody. Now I feel knowledgeable and happy.
Mwaka ujao, nitaanza shule ya sekondari katika idara ya afya na maendeleo ya vijana. Hapo baadaye, ninataka kuwatumikia vijana. Nikimaliza elimu yangu, ndoto yangu ni kupata ajira ya kudumu. Pia ninataka kujifunza udereva na nipate leseni yangu ya udereva.
Next year I will start secondary school in the health and youth development section. In the future I want to become a youth worker. When I have finished my education, my dream is to get a permanent job. I also want to learn how to drive and get my driver’s licence.
Kama ningebaki Somalia, ninadhani ningekuwa mama mpaka sasa. Pengine ningekuwa na watoto wengi. Kama ningekuwa Somalia, nisingekuwa na fursa sawa kama nilizozipata mpaka sasa. Ninajihisi mwenye bahati kuishi Norwei.
If I had stayed in Somalia, I think I would have been a mother by now. Perhaps I would already have many children. If I had been in Somalia, I would not have had the same opportunities as I have had now. I feel lucky to live in Norway.